Alhamisi 12 Februari 2026 - 06:00
Sherehe ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu imefanyika katika makazi ya ubalozi wa Vatican

Hawza/ Sherehe ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu imefanyika katika makazi ya ubalozi wa Vatican, huku baadhi ya maafisa wa Vatican na mabalozi kadhaa pamoja na wakuu wa uwakilishi wa nchi mbalimbali wakihudhuria.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, sherehe ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ilifanyika katika makazi ya ubalozi wa Vatican. Baadhi ya maafisa wa Vatican na mabalozi kadhaa pamoja na wakuu wa uwakilishi walishiriki.

Tofauti ya mkutano wa mwaka huu na miaka iliyopita walikuwepo watu watatu miongoni mwa wawakilishi wa Kikristo katika Bunge la Ushauri la Kiislamu, ambao katika hotuba zao mbele ya wahudhuriaji walifichua habari za uongo za vyombo vya habari vinavyohusishwa na ubeberu na utawala wa Kizayuni, na wakaeleza kwa uzuri hali halisi na matukio ya kweli ya maendeleo ya hivi karibuni nchini.

Inafaa kutajwa kwamba; kabla ya kuanza kwa hafla hiyo, walifanya mkutano wa waandishi wa habari pamoja na mashirika kadhaa ya habari na vyombo maarufu vya habari, na wakazungumzia kuhusu uhuru wa dini na haki za wafuasi wa dini na madhehebu yote nchini kwa mujibu wa katiba. Pia walijibu maswali ya wanahabari kuhusu idadi kubwa ya makanisa na sehemu za ibada, uungaji mkono wa serikali kwao, pamoja na shule na kusomwa Injili katika vituo vya elimu badala ya Qur’ani, kitabu kitakatifu cha Waislamu, na masuala mengine; jambo lililosababisha mshangao na butwaa kwa wanahabari hao.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha